DKT JUMA MALIK AKIL AFANYA ZIARA KATIKA OFISI ZA ZIAAT

POSTED ON: 04-02-2026

Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt Juma Malik Akil leo tarehe 04 Februari. 2026 amefanya ziara katika Ofisi za ZIAAT na kuzungumza na Wajumbe wa Bodi na Watendaji wa taasisi hiyo Mhe. Waziri ameeleza kuwa ZIAAT ni taasisi ya kitaaluma ambayo mpka sasa ina miaka miwili tu lakini imefanya mambo makubwa ikiwa ni pamoja na kusajili jumla ya Wanachama 810 pamoja na kuanzisha Mitihani ya Taaluma ya Kodi Aidha, Dkt Juma ameendelea kueleza kuwa ZIAAT inapaswa kujitegemea ili kufikia malengo ya kuanzishwa kwake Pamoja na mambo mengine Mhe. Waziri ameitaka ZIAAT kusimamia taaluma za kodi na Ukaguzi kwa umakini ili taaluma hizo ziendelee kufanya kazi kwa ufanisi ikiwa ni pamoja na kuwapatia mafunzo wanachama wake